Tuesday, July 10, 2012

Ziara ya akina Misosi yapata pigo, Soggy aumia mguu kwenye mtumbwi



Wakati ziara ya wakongwe wa muziki wa Bongo Flava nchini, Soggy, D-Knob na Bwana Misosi ikiwa haijamaliza hata wiki moja, imepata pigo baada ya Soggy kuteleza kwenye mtumbwi kwenye visiwa vya Ziwa Victoria, wilayani Sengerema, na kuumia.
Katika ajali hiyo Bwana Misosi tuliyeongea naye kwa simu amesema begi moja limepotea.
Kwa sasa wao, yaani Misosi na D-Knob wapo wilayani Sengerema, mkoani Mwanza, huku Soggy akiwa wilayani Muleba, Kagera kwa baba yake.
“Baada ya kuanguka kwenye mtumbwi na kuumia mguu tumeamua kusitisha show za visiwani kanda ya ziwa.Niko kwa Mzee Ngaiza-Muleba nakula matoke tu,” ameandika Soggy.
Misosi na D-Knob waliobakia wilayani Sengerema wamesema wamelazimika kusitisha show zao kwa siku sita na tayari wameshapiga show tatu.
Wameongeza kuwa kituo kinachofuata ni Mwanza mjini ambapo Soggy ataungana nao huko kuendelea na ziara yao ya kanda ya ziwa.

No comments:

Post a Comment