Exclusive: Fid Q aongelea lengo la Hip Hop Darasa
Kila jumamosi,Fareed
Kubanda huendesha darasa la hip hop la hiari jijini Dar es Salaam ambapo sasa
limeanza kuwa maarufu. Leo tumeongea kwa simu na Fid Q kutaka kujua nini
madhumuni ya darasa hilo na haya ni maelezo yake.
“Kwa haraka
haraka hip hop darasa maudhui yake ni kuwafundisha vijana wawe na positive
thinking na attitude kwa jamii, yaani wawe na fikira zilizopo katika mstari ulio
sahihi na hata kitabia, kwahiyo tunawajenga hivyo kupitia muziki wa hiphop.
Hip hop
darasa so far ina wanafunzi kama hamsini hivi na katika hao wanafunzi hamsini,
arobaini ni watoto wa mtaani wote. Ninapoingia darasani mimi kama mwalimu,kuna
vitu vingi sana najifunza. Kuna wengine wanakuja darasani hawajui kuandika
lakini wanarap vizuri, kuna wengine wanakuja darasani hawajui kusoma lakini
wanarap vizuri kwahiyo, tunafundishana mpaka kusoma na kuandika.
So far so
good, tuna wanafunzi kama kumi wameimprove vizuri na baadaya mwezi mmoja naweza
nikaanza kuwaonesha kwa watu kwamba hawa ndo wameimprove.
Mimi nafundisha
somo la hip hop lakini kuna wawezeshaji wengine kama Churchil ambaye ni mtaalam
wa masomo ya kujielewa na masuala ya leadership.”
No comments:
Post a Comment