Tuesday, June 12, 2012

Sneakers za Kanye West zinauzwa TZS Mil.130 mtandaoni


 
Mashabiki wanaotegemea kununua mapema pair ya viatu vya Kanye West viitwavyo Air Yeezy 2 Nike, wanaweza kuanza kufikiria kuomba mkopo benki ili kumudu bei yake!
Mpaka sasa viatu hivyo vinapigwa mnada kwa zaidi ya $90,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 130!.
Licha ya bei yake ya reja reja kuwa ni $245 sawa na shilingi 377,300, dau la pair moja limepanda hadi kufikia $100,000.
Uiagizaji wa kabla ya kuanza kuuzwa rasmi kwa viatu hivyo (pre-order) umefikia hadi $90,100 kwenye mtandao wa eBay.
Ingawa Kanye West, amekuwa akivaa viatu hivyo kwa miezi sasa, uuzaji rasmi wa viatu hivyo vya Nike unaanza kesho, June 9 na kuuzwa kwa $245. (ABC News)
Hata hivyo sneakers za Air Yeezy 2 zitakuwa chache tu kwenye store shelves.
 
Nike inasema itatoa viatu kuanzia pair 3,000-5,000. Japo kesho ndo vitaanza kuuzwa, mashabiki wameshaanza kujipanga kwenye maduka kadhaa yatakayokuwa yanaviuza nchini marekani (Philly)

No comments:

Post a Comment