Tuesday, July 10, 2012


Tundaman ataka Milioni 100 ili ajiunge na Watanashati



Jitihada za Ustaadh Juma wa Watanashati kumtaka Tundaman awatose Tip Top Connection na ajiunge naye zimegonga mwamba.
Hiyo ni baada ya Tundaman kumwambia ili ajiunge na Watanashati ni lazima aweke mezani dau la shilingi Milioni 100 cash!!!
Akiongea leo na East Africa Radio kwenye kipindi cha Power Jams, Tunda amesema Ustaadh Juma ameshamtumia watu zaidi ya wanne kumpelekea ujumbe wake uliokuwa ukimpa ofa ya shilingi milioni 10 ili ajiunge na Dogo Janja, Suma Mnazaleti na wasanii wengine kwenye kambi yake ya watanashati.
Tunda amesema Ustaadhi huyo amepitia kwa watu wengi akiwemo producer wake Manecky ili wamamshawishi ajiunge na watanashati.
Amedai kuwa kama kweli wana nia ya kumchukua basi wampe dau hilo ili ahakikishe kuwa anagawa kiasi kwa Babu Tale, Abdul Bonge wa Tip Top na familia yake ili aweze kuondoka kiroho safi.
Amesema akiondoka Tip Top ataacha pengo kubwa ambalo haliwezi kuzibika kwa shilingi milioni kumi.
Tunda amekiambia kipindi cha Power Jams kuwa Watanashati bado hawawezi kuleta impact yoyote nchini kutokana na wasanii waliopo na ndo maana wanamhitaji.
Unahisi Tundaman ana thamani ya shilingi milioni 100?

Picha; Zitto Kabwe akutana na Kigoma All Stars

Fid Q Rocks Vodacom Wanjaja Music Tour, Mtwara.



Hundreds of Wajanja Music Tour fans in Mtwara were thrilled on Sunday evening by music star  Farid Kubanda, popularly referred to as Fid Q, forcing him to stay on stage even after his performance had ended.
The excited fans screamed and cheered Ngosha!Ngosha!Ngosha!as Fid Q took to the stage a few minutes after fellow star, Diamond, finished his show, and gave security guards a hard time to manage the fans who later pushed his car in excitement not wanting him to leave.


Other artists who took the stage during the Mtwara music tour include Shetaa,Joh Makini, Ney wa Mitego and Mabeste.
While addressing the media, Matina Nkurlu, Vodacom Tanzania Public Relations Manager, said that the Wajanja Tour proceeds to Tanga this coming Sunday, at Mkwakwani stadium.
“Wajanja tour is set for “waja leo waondoka leo” in Tanga. The show really rocked Mtwara, so fans in Tanga better get ready for great entertainment from various artists this Sunday,” said Nkurlu.

Video: The Game akimpa kichapo 40 Glocc(real video)



40 Glocc ni rapper kutoka California ambaye kwa muda mrefu amekuwa akimtukana The Game kwenye YouTube na kujaribu kumharibia.

Sasa kwenye video hii ni kama bahati tu Game akakutana na adui yake live kitaani (ndege tunduni) na kumpa kichapo ambacho hakika hatokisahau katika maisha yake.

Video haipo clear sana lakini ukiiangalia yote utaelewa kilichofanyika. 

Imesambaa sana kwenye internet na 40 Glocc amesema hatofungua
mashtaka.

Lady Gaga awapa zawadi nzuuuuuuuri mapaparazi

New Music: Sheila Kwamboka (BBA 2008 na 2010) - Yours



Kwa wapenzi wa Big Brother jina la Sheila Kwamboka aka Kwambox sio geni. Alianza kujulikana mwaka  2006 aliposhinda taji la Miss Tourism Kenya. Baada ya hapo alifanya kazi kama ripota kwenye kituo cha runinga nchini humo mwaka 2008.

Mwaka huo huo akaiwakilisha Kenya kwenye Big Brother Africa na kisha kurejea tena mwaka 2010 kwenye Big Brother Allstars.

Kwa sasa anafanya muziki, muigizaji na muongozaji wa filamu.

Video: Idols (Afrika Kusini) 2012, Thabz akiimba!

Video: Davido na Playback mwanzo mwisho, Stargame Eviction show



Jumapili iliyopita msanii chipukizi wa Nigeria, aliyejipatia umaarufu ndani ya kipindi kifupi Davido, aliperform kwenye Eviction show ya Big Brother Africa Stargame.

Ngoma aliyoperform inaitwa Dami Duro ambayo kwa sasa ni club banger matata sana barani Africa. Ni ngoma kali to be honest!

Tatizo letu linakuja kwenye performance hii ambayo tunaweza kuiita ya kitoto. Labda sisi tunasikia vibaya, lakini hata macho hayadanganyi tukionacho kwamba kijana alikuwa akisynch mwanzo mwisho.

Tunafahamu kuwa show za Big Brother hazisindikizwi na live band hivyo wasanii huimba kwa kutumia beat chorus. Yaani msanii anaimba live kwenye sehemu ya verse tu na zile back alizoweka studio ndo zinaweza kubaki kwenye beat kumsupport.

Lakini kwa show ya Davido masikio hayatudanganyi kuwa tunachosikia mwanzo hadi mwisho wa performance yake ni vocal tamu za studio na yeye akiruka ruka tu na mpambe wake.



Tena tunahisi mic zilikuwa zimezimwa kabisa sababu hasikiki akiimba chochote! Hakuna haya yoyoyoyo! Damn! Why holding a mic if you don't even sing!! Bahati yake ni kwamba ngoma ni kali, watu wanaipenda kwahiyo ilikuwa shangwe tu mjengoni na tena ukizingatia sound system ya nguvu iliyofungwa mle ndani, aahh ni raha tu.

Lakini mtindo huu unaoendekezwa na waandaji wa Big Brother una hasara kubwa kwa wasanii wenyewe. Davido ni msanii mkubwa kufanya performance kwa ‘kusynch’ (kujifanya unaimba wakati cd ya wimbo original inaimba).

Huo ulikuwa ni muda kwake kudhihirisha kuwa si msanii wa studio tu bali anaweza kufanya show kwa sauti yake halisi na watu bado wakaifurahia.

Pamoja na umaarufu wake, sisi tunasema hii ndio performance mbaya kabisa tangu show hizo zianze kwenye shindano la Big Brother.

No comments:

Post a Comment