Thursday, August 2, 2012


New Music: Navio ft Nonini, Chameleon & Uganda All Stars – Dream Remix


New Music: 2face, D'banj, M.I Abaga, Wizkid & Tiwa Savage - Let's Get This Party Started

Video ya Leka Dutigite:Siku mbili tu lakini ina views 11,123 Youtube



Let’s be honest, video hii imevunja rekodi za ngoma za Bongo kwenye Youtube! Ndani ya siku mbili tu tangu iwekwe tarehe 31 July, 2012 kwenye mtandao huo tayari imeangaliwa zaidi ya 11,232 and counting!

Amini usiamini kufikia namba hiyo ndani ya siku mbili sio rahisi hata kidogo.

Acha tuchukue mfano uelewe nini tunachomaanisha. Video ya Ay ft. Marco Chali – Party Zone iliwekwa tarehe 15 July, 2012, hadi leo ina views 15,613. 

Video ya Sihitaji Marafiki ya Fid Q ft. Yvonne Mwale iliwekwa tarehe 2 July, 2012 na mpaka sasa ina views 9,463. Hiyo ni mifano tu inayokupa picha ya jinsi gani video hiyo itakuwa imeangaliwa ikifikisha mwezi mmoja.

Kitu kingine kinachovutia kwenye video hii ni pale Diamond anapoonekana akiwa amekaa karibu na dada yake pamoja na Wema Sepetu upande wake wa kushoto. Ni rahisi kugundua jinsi connection iliyokuwepo kati ya wapenzi hao wa zamani kiasi ambacho kinatoa jibu la wazi kuwa huenda ni kweli wamerudiana.
Angalia jinsi Wema alivyoshika mikono ya Diamond

Haya bi baadhi ya maoni kwenye video hiyo.

“I'm a real 100% Muha from Marumba, Kasulu, Kigoma but born and rose in Dodoma, I real like the song, this is what we want. Kigoma is a historical region but among of the region on which the economy is developing very slowly. " Abhantu bhakunda bhikongwa" but why we are poor?. Let all of us promote our region by any means. I'm eager to know that water fall location so that we can generate a micro if not a mini hydropower, Mr. Zitto or anyone can you direct me where i can find it.”

“Wanna like this video like 1000 times, thou i wasn't raised in KGM ila my blood has all elements of muha from manyovu, Kasulu. Nice song, nice idea and by the way u guys have shown other artists that love and unity is all we need. Ya'll keep doing what u gotta do to rep the mamaland KGM #Proud Kigoma.”

Picha ya siku: Peter Msechu, mwanae na baby mama!

EBSS kuanza kuruka jumapili hii kupitia ITV


Baada ya kuzunguka karibu mikoa yote kusaka vipaji vya kuimba, jumapili hii ya August 5, show za usahili za Bongo Star Search, zitaanza kurushwa kupitia ITV.
Washiriki wa EBSS Dar wakipata maelekezo kadhaa mapema leo (August 2)
\
Usahili huo unamalizia kufanyika jijini Dar es Salaam.
Mshindi wa mwaka huu ataibuka na kitita cha shilingi milioni 50.

Leona Lewis sasa kurap, amwambia Minaj: 'I'm coming for you Nicki!'


LEONA Lewis ameamua kujaribu bahati yake kwenye rap na albam yake mpya itakuwa imejaa michano tu.

Na mrembo huyo anajiamini kuwa atakuwa tishio kubwa kwa Nicki Minaj ambaye hana mpinzani kwa sasa kibiashara.

Mwanamuziki huyo wa Uingereza kwa sasa anamalizia malizia ngoma yake mpya ambayo anasema itakuwa tofauti kabisa.

Akiongea na gazeti la The Sun Leona amesema : "On my new album I will be rapping. I've discovered my voice for rapping.


"I could probably go up against Nicki Minaj now. I'm actually that good, so I'm coming for you Nicki! London style MCing."

Makala: Makosa yanayofanywa na wasanii wetu wakubwa

Rama Dee

Na Emmanuel Msigwa aka DJ Msigwa: Radio Journalist, Presenter ,Radio DJ & Club DJ, Pride Fm Mtwara

Nimekuwa nikiumia sana kuona wasanii wetu ambao tunawaita wasanii wakubwa, hapa nina imani unanielewa ninaposema “wasanii wakubwa” na nikisema nitaje majina nahisi orodha itakuwa ndefu lakini leo naomba nimtaje mmoja ambaye amekuwa sehemu ya wasanii ambao wanazikosea sana kazi zao hasa video za nyimbo zao na nitaeleza wapi wanakosea,nini wanatakiwa kufanya ili muziki wetu uweze kusonga mbele zaidi ya hapa ulipofikia.

Leo naomba nianze na RAMA DEE, huyu ki ukweli ni mmoja kati ya wasanii wa Tanzania ambao mimi nawaona wana vipaji vya hali ya juu katika aina ya muziki wanaoufanya hasa wanapofanya “rhythm and blues “ yaani r&b nani ambaye hajui sauti nzuri ya jamaa huyu? Nani hajui ngoma kali zilizofanywa na jamaa huyu? Na ni nani pia ambaye haujui ngoma kali alizoshiriki kuzipamba kwa sauti yake tamu? Je unaikumbuka J.O.S.E.P.H ya Prof Jay? Unaikumbuka  ngoma kama RIDHIKA NAMI, SARA,NAJUA na SIYO WAOAJI? Bila shaka hizi si ngoma ngeni masikioni mwako…kifupi jamaa anaweza sana mimi ni mmoja kati ya mashabiki wake!

Kwa sasa jamaa ametoka na ngoma yake mpya inayoitwa KUWA NA SUBIRA ambayo ndani wameshirikishwa rafiki  zake wa kitambo MAPACHA, umewahi kuisikia ngoma hiyo? Kama bado sikiliza ngoma hiyo! Ngoma haina hata mwezi  toka ilipotoka yawezekana wiki mbili tu au tatu toka ilipoachiwa, nakumbuka mimi nilikuwa mmoja kati ya watu waliandika katika “wall” zetu za facebook niliusifia sana wimbo huo na kwangu mimi naona MAPACHA walistahili kuwepo katika wimbo huo.

Licha ya uzuri wa wimbo huo bado napata mashaka ubora wa wimbo huo unaweza kuwa wa muda mrefu? Je ngoma hiyo inaweza kukaa miaka hata kumi (10) ukahit kama ilivyo sasa? La hasha!........sidhani! nakiri tena sidhani! Kwanini? Unaikumbuka  THRILLER ya MICHAEL JACKSON? Unajua ngoma hiyo ilitolewa mwaka gani? Kwa taarifa yako ni kwamba mtayarishaji wa  muziki aitwaye QUINCY JONES alitengeneza ngoma hiyo kupitia album iliyopewa jina hilo mwaka 1982 je ni miaka mingapi sasa? Je umewahi kuona video ya ngoma hiyo? Bila shaka ndiyo!......sasa basi kama haufahamu ni kwamba ubora wa video hiyo ndiyo uliifanya ngoma hiyo kung’ara mpaka sasa kwa nini wasanii wetu hawajifunzi kupitia wao? Je awapati nafasi ya kujifunza kupitia ngoma fulani au ndiyo kusema wanakurupuka?

Je umepata nafasi ya kuangalia video ya wimbo huo wa RAMA DEE wa KUWA NA SUBIRA? Ni video nzuri kwa maana ya rangi,mandhari na uchanganyaji wake wa picha! Vipi kuhusu  wahusika? Vipi kuhusu story board ya wimbo huo? Sijui gharama ya wimbo huo lakini nina imani tena ya dhati kabisa kuwa video hiyo itaishusha sana thamani ya  ngoma hiyo kwa maana ya audio yake, fumba macho wakati unaisikiliza ngoma hiyo halafu wakati huo huo tazama video yake! Je kuna uhalisia wowote? Umewahi kuusikiliza wimbo wa SAME GAL wa R.KELLY & USHER RAYMOND?  Umewahi kuona video yake?

Si huo tu ni nyimbo nyingi sana ambazo naweza kutolea mfano ni kweli, RAMA DEE hajui hicho? Hakuna watu wa kuwashauri wasanii wetu? Au wasanii wenyewe hawataki kuwashirikisha watu wenye upeo wa mambo hayo? Inasikitisha sana! Ki ukweli ngoma nyingi kali za jamaa ambao ni audio zinaangushwa na video zake si pekee yake bali wapo wengi nitawaelezea siku nyingine!

Wakati fulani mwaka 2011 nilipata kushiriki katika mradi mmoja wa waandishi wa habari nchini Ujerumani na kukaa huko kwa muda kuna kitu kimoja upande wa sanaa nilichojifunza kule moja ya vitu hivyo ni namna wanavyosimamia kazi za sanaa na pili ni namna kazi hizo zinavyotoka mathalani album ya msanii au wimbo wa msanii utakaoucheza klabu za disko si ule utakaousikisiliza redioni na kadhalika ni tofauti na utakaouona katika video na wala hautafanana na ule wewe utakaoununua tofauti uanzia katika midundo “beats” baadhi ya mistari “lyrics”  wakati mwingine hutofautiana katika melody zake, hivyo  ndivyo wenzetu wanavyofanya kikubwa zaidi ni kwamba nyimbo zao ubebwa na ubora wa video zake na ndiyo maana wasanii wengi wa Marekani utoa kwanza video za nyimbo zao kabla hajasambaza audio zao.
Tungependa kuona video za wasanii wetu zibebe pia theme ya wimbo husika, kama mtu akizungumzia suala la kumsifia mpenzi/mke wake kwa mapishi mazuri basi tuone kipande cha muhusika akipika na si kuona anachota maji au kuona tabasamu lake!.............ndugu zangu, rafiki zangu wasanii badilikeni hili kazi zenu zidumu miaka hata 30 zaidi ni kuboresha video za NYIMBO ZENU!

Manecky azungumzia shutuma ya kuuza beat mara mbili

Producer wa AM Records, Manecky leo ameizungumzia kashfa inayomkabili ya kuwagonganisha wasanii wawili wa hip hop aliowapa beat moja.

Wasanii hao ni Izzo B na mwingine aitwaye Brian huku beat inayogombaniwa ikiwa ile ya wimbo wa Izzo B, ‘Mwaka Jana’.

Akihojiwa kwenye kipindi cha XXL  cha Clouds Fm, Manecky amekanusha kumuuzia beat Briain kwa shilingi laki 3 kama msanii huyo alivyosema jana na kwamba alimpa bure kwakuwa msanii huyo mara nyingi huenda kwenye studio hiyo na tayari amesharekodi nyimbo kadhaa kwenye studio hiyo.

Akielezea namna beat hiyo ilivyotengenezwa  Manecky amesema kuna siku alienda Maisha Club ambako alikutana na wasanii kadhaa akiwemo Izzo na kuwasalimia. Anasema baada ya kuwasalia kuna mtu mmoja maarufu ambaye hakumtaja jina alimskia akimdiss kuwa yeye sio producer nali ni producer viduku.

Baada ya kuambiwa hivyo manecky ajisikia vibaya sana kuamua kuondoka kwenye club hiyo.


"Nilimaindi kiukweli, cha kufanya sikurudi hata home , nikaenda studio, na beat nikagongea pale, ile siku nakumbuka nilifanya beat kama tatu, moja wapo ikiwa ile, ambayo the same beat, kama baada ya siku mbili tatu , tukawa tumeitwa kwenye vikao vya Kili Music vile, nikampa Izzo. Na that beat natengeneza moyoni mwangu. akilini mwangu nilikuwa natengeneza beat kwaajili ya Izzo B.

Manecky anasema baadaye ndipo Brian alikuja kusikia ile beat na yeye akaipenda na kuifanyia wimbo kwa maana kwamba baadaye producer huyo angekuja kuweka vocal zake kwenye beat nyingine na tayari alikuwa amemwambia kuwa ile ni beat ya izzo.

Msikilize zaidi kwenye maongezi hayo.

REINCARNATED (ft. Snoop Dogg): Official Documentary Trailer

Eddo wa Ebony Fm azungumzia sababu ya kumpiga msanii wa Iringa


Jana tuliandika habari kuhusiana na msanii wa Hip hop wa Iringa, Man Kichefu kudai kuwa amepigwa na mtangazaji wa Iringa Eddo Bashir. Leo tumezungumza kwa urefu na mtangazaji huyo kuchukua yale yaliyopo kwa upande wake.

Eddo amesema kilichotokea anakifananisha na kitendo cha mdogo kujaribu kumtukana mkubwa kwa makusudi ili  kumuona mkubwa atafanyaje.

“Yule mtoto kimuziki mimi nimekua naye, mimi ofcourse nilikuwa simjui lakini historicaly nimeambiwa kuwa kuna mtu mmoja anaitwa Meki ambaye kamdissi pia kwenye hiyo track.”

Anasema Meki ndiye aliyempeleka Man Kichefu kwa Amba (producer) ambaye alimfanyia wimbo bure iliyoitwa ‘Utanikumbuka’ ambapo Amba aliimba chorus.

“Ile track imekuja mikononi mwangu, nikaiona nzuri nikawa naipa airtime ya kutosha simjui na wala sijawahi kumtafuta,”anasema Eddo.

Kutokana na kitendo hicho Eddo anasema Man Kichefu alifanya jitihada za kumtafuta ili amshukuru kwa kumchezea ngoma yake hiyo.

“Mimi ndo mtu wa kwanza kumuita yule mtoto genious, na ana nyimbo zaidi ya tatu na nimempa interview zaidi ya saba,namfeel kwasababu anaweza kuandika.

Hakuna siku ambayo nimesema naomba kitu chochote kutoka kwake pamoja na support niliyokuwa nampa, lakini kwenye nyimbo anaimba, mimi naua muziki wa Iringa, mimi nachukua hela za wasanii kitu ambacho mimi nina watoto ambao wananifuatilia ninachokifanya na wanacatch vile ambavyo vimeimbwa mule.
Mimi nahangaika na muziki wa Iringa karibu nakuwa chizi na watu wanajua, hamna mtu ambaye hajapita kwenye mgongo wangu hata akifanya interview asahau kunishukuru. Piga story na Mike, Mike anatoka kwenye mgongo wangu, piga story na Squeezer, piga story na Dataz, piga story na Zay B,” Eddo aliongeza.

Mtangazaji na DJ huyo anasema baada ya kutopendezwa na kitendo cha Man Kichefu, aliamua kumuita studio ambapo hakukataa na kuanza kumkubusha alikomtoa. Hata hivyo anasema msanii huyo aliendelea kuonesha dharau kwa kumsukuma, kitendo kilichomuudhi.

“Kiukweli nilifanya kitu ambacho sikuwahi kukitegema kukifanya, kwasababu pia mimi ni binadamu wa kawaida, nilikuwa na jaziba. Kweli yule mtoto nimemchapa, sio kidogo, honestly na Mungu anisamehe, nimempiga sana yule mtoto … sana.”

Eddo pia amemshangaa Man Kichefu kwa kitendo chake cha kumdiss Amba kwenye wimbo huo wakati ni producer aliyemsaidia kwa mengi.

Hata hivyo amechukua nafasi hiyo kuwaomba radhi mashabiki wake ambao hawajamwelewa kutokana na kitendo chake hicho cha kumpiga Man Kichefu.

Sikiliza interview yote hapa:

Kwa upande wa shutuma zilizotolewa na msanii hiyo kuwa Ebony Fm haitoi support kwa wasanii wa Iringa, mkurugenzi wa vipindi wa kituo hicho cha radio hiyo, Renatus Kiluvia aka Bizzo amekanusha kwa kudai kuwa hazina ukweli wowote.
Bizzo
Bizzo amesema Ebony Fm ina vipindi viwili vya muziki wa Bongo Flava ambapo kimoja ni kwaajili ya nyimbo zote kwa ujumla na kingine kikicheza nyimbo za wasanii wa eneo inaposikika redio hiyo katika mikoa ya Iringa, Mbeya, Dodoma na Morogoro, Rukwa na Njombe.

New Music: Mad Ice & Mika Mwamba - Ninatamani

Picha: The making of video for Live it up - Tulisa ft Tyga

New Music: Pah One - Ghetto

New Music: Jose Chameleone - Moto Moto


New Music Video: Leka Dutigite - Kigoma All Stars

New Music Video:Flavour ft. Fally Ipupa - Kwarikwa Remix

Diamond asumbuliwa na kifua alazwa kwa muda


Hii ni picha ya Diamond akiwa hospitali baada ya kubanwa ghafla na kifua na hivyo kwenda kufanyiwa uchunguzi ili kujua tatizo. Kwa mujibu wa Ommy Dimpoz ambaye ni mshikaji wake wa karibu tayari msanii huyo amesharuhusiwa lakini majibu ya vipimo vyake yatatoka kesho. 


Miezi ya hivi karibuni Diamond amefululiza kufanya show katika mikoa mbalimbali bila kupata mapumziko ya kutosha na huenda hiyo ndio ikawa ni sababu.


Kupitia Twitter Diamond ameandika "Dah hali yangu si nzuri, naumwaaa."


Tunamwombea Diamond apone haraka.

Breaking:Wasanii wapiga marufuku matumizi ya ringtone zao, wayapa makampuni ya simu siku saba



Umoja wa wanamuziki wa Bongo Flava, Rhumba, Dance, muziki wa Injili na aina zingine leo umetoa agizo kwa makampuni yanayouza miito ya simu nchini pamoja na makampuni ya simu kuiondoa miitio hiyo ndani ya siku saba kuanzia leo mpaka pale watakapokubaliana mikataba mipya.

Katika barua hiyo iliyoandikwa kwenda kwa waandishi wa habari na iliyosainiwa na wasanii zaidi ya 150 nchini, wasanii hao wameyataka makampuni ya simu kuondoa matangazo ya ringtone hizo kwenye radio, magazeti, tv, website na kwenye ujumbe mfupi wa simu.

Hatua hiyo imechukuliwa na wasanii hao baada ya kubaini kuwa makampuni ya simu yanawanyonya kwa kiasi kikubwa kwa kuwalipa chini ya asilimia 10 ya mauzo ya ringtone hizo huku yenyewe yakibaki na zaidi ya asilimia 80.

Wiki iliyopita mbunge wa Kigoma Zitto Kabwe aliliibua suala hilo bungeni na kudai kuwa imeundwa kamati itakayoangalia upya utaratibu wa mauzo ya ringtone.

Press Release ndio hii.

YAH: KUFUTA MIKATABA NA KUSIMAMISHA KUUZA MUZIKI WA BONGO FLEVA,GOSPEL,DANSI NA TAARABU KWENYE MITANDAO YA SIMU.
Husika na kichwa cha habari hapo juu,
Kwa ujumla wetu sisi Wasanii toka Tanzania tunaofanya muziki wa Gospel, Rhumba , Taarabu pamoja na Bongo fleva tumeamua kutoa agzio kwenu la kusimamisha mauzo ya kazi zetu za muziki katika mtindo wa Ringtone na Callertunes katika mitandao ya simu ya Vodacom, Zantel,Tigo na Airtel na kufuta mkataba tuliosaini kati yetu sisi Wasanii na Kampuni yako mpaka hapo tutakapokaa sisi kama wasanii, nyinyi kama wasambazaji wa muziki wetu, pamoja na Mitandao ya simu ili kuzungumzia namna mpya ya sisi na nyinyi tutakavyofanya kazi.
Sababu ya sisi Wasanii kusimamisha na kufuta mikataba kati yetu na wanaofanya biashara ya kuuza maudhui yetu ni pamoja kampuni husika kushindwa kuweka wazi taarifa za mauzo ya nyimbo pamoja na kutolipa katika muda husika kama ilivyoanishwa katika mikataba husika.
Sababu ya pili ni mitandao ya simu kuchukua kiasi kikubwa cha fedha ambacho ni asilimia themanini ya mauzo yote ya maudhui yetu, jambo hili linatuumiza na limetufanya tuendelee kuishi kwa kutegemea aina moja ya pato toka kwenye shoo.
Hivyo tumeziagiza kampuni zote zinazofanya kazi ya kuuza maudhui yetu kutoa maelekezo kwenye mtandao husika kuwaelekeza kusimamisha mauzo ya kazi zetu za sanaa ndani ya siku saba kuanzia leo tarehe 30/07/12 ikiwa pamoja na kusimamisha matangazo yote yanayotangaza mauzo ya kazi zetu kwa njia ya Television , Radio , blogs, website, Magazeti na Ujumbe Mfupi wa maneno mpaka hapo tutakapofikia muafaka.
Jumla ya wasanii 153 wameshasaini barua hizo na wengine wanaendelea kusaini.
Mwisho tunawashukuru kwa ushirikianao wenu, na tunaambatanisha sahihi zetu ili kuonyesha uthibitisho wa umoja wetu katika jambo hili.
Asante.

New Music: Izzo B ft. Belle 9 - Utarudishwa

Picha za Arnord Kayanda alipoenda kutoa mahari!

Exclusive: Mtangazaji wa Ebony FM Iringa ampiga msanii wa Hip Hop

Man Kichefu

Kupitia ukurasa wa Facebook msanii wa hip hop wa mkoani Iringa Man Kichefu, leo ameandika, ‘jana nliitwa na eddo ebony.fm cha kushangaza alinivamia na kuanza kunipiga akidai nimemchafua! Poa mi sina noma ila nachoweza kusema its only the weak need to prove his strength through force! My mom hits more than anyone I ever met!”

Kufuatia status hiyo tumempigia simu Man Kichefu ili atueleze sababu ya yeye kupigwa na mtangazaji huyo.

“Kuna harakati fulani za muzki wa nyumbani hapa, unajue eeh, jamaa (Ebony Fm) wanatudiss sisi wasanii wa hapa. Kwahiyo kitu kilichokuja kufanyika kuna ngoma fulani sababu sisi kuna studio yetu tumefungua , tumejichanga tu mimi na mshikaji wangu tumefungua studio ,tumetengeza ngoma moja kwahiyo hiyo ngoma tuliyoitengeza inaitwa ‘Himaya ya Mkwawa’ inaelezea historia ya muziki wa Iringa na watu wa Iringa wale wanausuport muziki na wasio usupport. Baada ya ngoma hiyo niliiyoifanya sababu nimeiweka tu kwenye internet jamaa wakaichukua ile ngoma kitu kama wakaisikiliza hivi lakini mimi nikawa sijui.

Nikawa napewa tu taarifa kuwa jamaa anakutafuta kaongea sana redioni. Mwisho wa siku juzi akanipigia simu mimi nikaipokea tu kwa roho safi, ‘vipi  bro, fresh fresh’ akaniambia ebana na shida na wewe njoo ofisini.
Nikamwambia poa mimi nikaenda tu kwa roho safi. Ndio hivyo yanii nimeenda ofisini jamaa akaniita akaanza kunitukana pale anadai nimemchafua, kanivamia akaanza kunipiga.

Na baadhi ya wafanyakazi wengine yaani walikuja wakawa wananishika wananiambai ebana twende huku tukaongee. Pale ofisini kwao kuna sehemu moja nyuma ya ofisi kuna kibanda cha kupumzikia hivi, akaniita pale njoo tuongee.

Nimefika hapo ndo akaanza kunishambulia sasa mimi nikaona hili eneo si zuri sababu ni nyuma ya ofisi, nikakimbia nikaja nyuma ya ofisi.
Nimekuja mbele ya ofisi baadhi ya wafanyakazi wenzake wakaja wakanishika bana twende huku wakawa wananirudisha tena kule ambako jamaa alikuwa ananipiga yaani!
Eddo mtangazaji wa Ebony Fm
Kitu nilichokifanya mimi, nimefungua kesi polisi kwasababu ya ulinzi wangu wa mbele au kitu chochote kitakachoenda kule mbele lakini pia mimi sitaki nimfunge ama nimfanye lolote yaani.”

Tumemtafuta Eddo ili aeleze kwa upande wake lakini simu yake haipatikani.


Sikiliza interview yote hapa


Huu ndio wimbo wa Man Kichefu ulioleta mgogoro.

Monday, July 30, 2012

Ben Pol alijua ‘Baadaye’ ya Ommy Dimpoz itakuja kuwa hit


Mara nyingi wasanii hupata fursa ya kusikiliza nyimbo za wenzao zinapokuwa kwenye hatua ya kutayarishwa.
 
Ben Pol aliusikia wimbo wa Ommy Dimpoz kabla hata ya kutoka na kumwambia kuwa utakuja kuwa tishio.
 
‘Unakumbuka niliwahi kukuambia kuhusu 'Baadae ,ona bro ,sasa nchi yote inaimba 'Baaadaeee eeeh'...hongeraaaa!!!,” ametweet Ben Pol kumwambia Ommy Dimpoz.
 
“Nakumbuka broo thanxxx,” alijibu Ommy.
 
Baadaye ni wimbo wa pili wa Ommy Dimpoz kufanya vizuri baada ya kuhit pia na wimbo wake wa kwanza, Nai Nai aliofanya na Ali Kiba.
 
Katika hatua nyingine Ben Pol amekuwa msanii wa kwanza Tanzania kuzungumzia habari ya msanii maarufu wa Marekani Frank Ocean kujitangaza kuwa ni shoga.
 
“Frank ocean anatuweka watu kwenye wakati mgumu ,ametoa album kali huku amejitangaza kuwa yeye ni gay ,kumuacha kumsikiliza nayo ni ishu,da!” amesema.
 
Hata hivyo hitmaker huyo wa ‘Nikikupata’ na mshindi wa tuzo za Kili, anaamini kuwa scandal hiyo haimpunguzii uwezo wake katika muziki.
 
“Haishushi ,ila bado wabongo sisi hatuwaelewi mashoga (mimi mbongo pia) ,ameni-dissapoint kidizain flani ,ila he's a gud singr/writer.”
 
Album ya Frank Ocean, Channel Orange ilikamata nafasi ya pili kwenye chart ya Billboard 200 na nafasi ya kwanza kwenye Billboard R&B/Hip-Hop Albums chart, kwa kuuza kopi 131,000 katika wiki ya kwanza.

Olimpiki: Kidunda 'adundwa' na Mmoldova

Picha: Jason Derulo akiperform nchini Rwanda

Rachel K wa Uganda kujaribu bahati American Idol ijayo

Keko asainishwa na Sony BMG Africa



Tuliliona hili linakuja mapema mno kutokana na uwezo wa rapper huyu. Hatimaye kweli imekuwa hivyo. Rapper wa kwanza wa kike nchini Uganda kupenya kwenye mainstream, Keko amekula mkataba na record label ya Sony BMG Africa.

Keko amekuwa akiwasiliana na Sony BMG Africa na amekuwa akifunga safari za hapa na pale kwenda Afrika Kusini kuzungumzia mchongo huo. Habari njema ni kuwa rapper huyo anayetamba sasa na ngoma ‘Make You Dance’ amechukuliwa rasmi.

Kwa sasa Keko anajiandaa kufanya collabo na msanii wa Afrika Kusini Toya Delazy ambaye naye yupo chini ya Sony.

Keko anaungana na mkenya Xtatic aliyesainishwa hivi karibuni na label hiyo pamoja na Rose Muhando ambaye alichukuliwa mwaka jana.

Sinta na Nyoshi El Sadaat kuja na ‘The Return of JLO'



Mwanadada Sinta na mwanamuziki wa kundi la Fm Academia, Nyoshi El Sadaat wanakuja na filamu iitwayo The Return of Jlo.
 
Filamu hiyo inayoongozwa na muongozaji maarufu wa kampuni ya Steps Entertainment, Selles Mapunda itaingia sokoni mwezi September, 2012.
Kupitia website yake, Sinta ameandika:
 
“Jumamosi saa nne na robo usiku ndio itakuwa habari ya mujini pale movie yangu ya the return of jlo itakapoanza vibweka vyake katika station yako ya star Tv.Ni vipande tuu,mpango mzima ni mwezi wa tisa, si ya kukosa ikiingia madukani maana I’m back like  never went. Saa ni saa nne na robo usiku.Star Tv  na Sauda mwana wa Mwilima.Glory be to God.
Sinta na Nyoshi wakiwa kwenye scene
Hata hivyo baadhi ya wasomaji wa website yake wameendelea kumkejeli kama ilivyo kawaida.
 
“Subiri tukusifie we mbwiga …..uzinduzi waufanyia hollyowood au kule kwenu kimara????? Kuchamba kwingi kushika mavi na usijidai baharia kumbe wajiharia, kuwa msomi kama unavyojinadi,” aliandika mmoja.
 
Selles Mapunda na Sintah
Mwingine alisema,”Dah kweli wewe u r not creative, bingwa wa kucopy paste sasa hivi atamwambia baby yake amnunulie nyumba iliaoneshe kwenye tv, kubwa jinga hili limama linaloshindana na watoto.”

(Video) Justin Bieber ft. Big Sean – As Long As You Love Me [Sneak Peek]